Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 46 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 390 2018-06-07

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:-
Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano wakati wa kampeni aliwaahidi wananchi wa Itigi katika Jimbo la Manyoni Magharibi kusaidia kupunguza gharama kubwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mtakatifu Gaspar, pia kulipa mishahara yote ya watumishi, mgao wa dawa kutoka Bohari Kuu ya Dawa (MSD), vifaa tiba na kuongeza Madaktari Bingwa:-
• Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo?
• Je, Serikali haioni kuwa kwa sasa ni bora kujenga hospitali ya Serikali katika Halmashauri mpya ya Itigi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Manyoni Magharibi, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuboresha ushirikiano kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP) katika utoaji wa huduma za afya, Serikali inatoa ruzuku ya fedha kwa ajili ya kulipia mishahara ya watumishi pamoja na ruzuku ya dawa na vifaatiba. Jumla ya watumishi 50 wa Hospitali ya Mtakatifu Gaspar wanalipwa mishahara na Serikali ambao ni Daktari Bingwa mmoja, Daktari (MD) mmoja, Mteknolojia Maabara Mmoja, Madaktari Wasaidizi Wawili, Tabibu Wawili na Wauguzi 43.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, mgao wa dawa na vifaatiba kutoka Bohari Kuu (MSD) unaendelea kutolewa na Serikali. Katika mwaka wa fedha 2016/2017, kupitia MSD Serikali ilitoa dawa zenye thamani ya shilingi milioni 105.674 na mwaka wa fedha 2017/2018 hospitali ilipatiwa dawa zenye thamani ya shilingi milioni 114.671.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Itigi katika bajeti ya mwaka 2018/2019, imetengewa jumla ya shilingi milioni 600 kama ruzuku ya miradi ya maendeleo ili kuanza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya. Eneo la ujenzi wa hospitali lenye ukubwa wa ekari 50 limeshatengwa katika Kijiji cha Kihanju, Kata ya Tambukareli.