Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 45 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 386 2018-06-06

Name

Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:-
Lengo la Serikali ni kuhakikisha kila kijiji kinapata umeme wa REA; je, ni lini sasa vijiji vyote vya Jimbo la Busanda vitapata umeme?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Lolesia Jeremiah Bukwimba, Mbunge wa Busanda, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Busanda lina jumla ya Kata 22 na vijiji 83 ambapo kati ya hivyo 14 vimepatiwa nishati ya umeme; vijiji nane vitapata umeme kupitia mradi wa REA awamu ya tatu mzunguko wa kwanza ambapo vijiji vya Bugogo, Ntono, Ihega, Butobela na Ngula ni miongoni wa vijiji vitakavyonufaika na mradi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkandarasi wa Kampuni ya White City International Contractors Electrical Power Engineering Co. Ltd ameshaanza utekelezaji wa kazi za mradi na kazi hiyo itakamilika mwezi Juni, 2019.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya kupeleka umeme katika Jimbo la Busanda, itajumuisha ujenzi wa kilometa 21.44 za njia ya umeme wa msongo kilovoti 33 na kilometa 26 za njia ya umeme wa msongo 0.4 kilovoti, ufungaji wa transfoma 14 na uunganishaji wa wateja wa awali 404. Gharama za mradi ni shilingi bilioni 1.56.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, vijiji vitano vya Buyagu, Nyalwanzaja, Kamena, Nderema na Imalampaka vitapata umeme kupitia mradi wa ujenzi wa njia ya msongo wa 220KV wa Bulyanhulu – Geita ambapo Mkandarasi anatarajiwa kufika site mwezi Mei, 2018. vijiji 56 vilivyobaki vitapata umeme kupitia mradi wa REA Awamu ya Tatu, mzunguko wa pili unaotegemewa kuanza mwezi Julai, 2019 na kukamilika mwezi Juni, 2021. Ahsante. (Makofi)