Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 9 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 122 2018-09-14

Name

Maulid Said Abdallah Mtulia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. ZAYNAB M. VULLU (K.n.y. MHE. MAULID S. MTULIA) aliuliza:-
Serikali inafanya juhudi kubwa ya kuzuia biashara ya ukahaba kwa kuwakamata wauzaji na wanunuzi na kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria. Pamoja na jitihada hizo bado biashara hiyo haramu inaendelea kwa kasi ileile:-
Je, Serikali ina mpango gani mbadala wa kuzuia biashara hii haramu?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maulid Said Mtulia, Mbunge wa Kinondoni, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuwa kwa muda mrefu Serikali imekuwa ikipambana na watu wanaojihusisha na vitendo vya ukahaba nchini. Jeshi la Polisi limekuwa likifanya misako kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kwa kubaini na kukamata watu ambao wanajihusisha na vitendo hivyo ambavyo ni kinyume na maadili ya Kitanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la ukahaba ni suala mtambuka ambapo kulikabili kunahitaji ushirikiano wa wadau wengi. Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kupitia Jeshi la Polisi, imeandaa mkakati wa kushirikisha taasisi nyingine za Serikali kama vile TAMISEMI, Wizara ya Katiba na Sheria, Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii na kupunguza hatimaye kumaliza vitendo hivi ambavyo vinautia doa utamaduni wa nchi yetu. Aidha, mkakati huu unahusisha ujenzi, kutoa elimu ya madhara ya ukahaba, faida za ujasiriamali na kuwashirikisha viongozi wa dini katika kufundisha maadili.