Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 9 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 120 2018-09-14

Name

Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Primary Question

MHE. MBARAKA K. DAU aliuliza:-
Papa aina ya potwe (whale shark) ni samaki ambaye duniani kote anapatikana Australia na Tanzania katika Kisiwa cha Mafia tu:-
Je, ni lini Serikali itakuja na mpango mkakati wa kumtangaza samaki huyo pamoja na vivutio vingine vya utalii kama vile scuba diving na sport fishing duniani ili kuvutia watalii nchini?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbaraka Kitwana Dau, Mbunge wa Mafia, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, papa aina ya potwe (whale shark) anapatikana katika maeneo mbalimbali duniani hususan nchi zilizoko katika maeneo ya tropiki kama Australia, Taiwan, Pakistan, India, Ufilipino, Indonesia, Afrika Kusini, Kenya, Msumbiji na kwa Tanzania anapatikana katika Visiwa vya Mafia (Kilindoni), Pemba na Zanzibar. Samaki huyu ni mmoja kati ya samaki wakubwa sana duniani na uzito wake unaweza kufikia mpaka tani zaidi ya 20 na urefu kufikia zaidi ya mita nane na hivyo kuwa kivutio kikubwa cha watalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara kupitia Bodi ya Utalii Tanzania inaendelea kutangaza vivutio vya utalii ndani na nje ya nchi vikiwemo vivutio vya Wilaya ya Mafia ikijumuisha papa aina ya potwe kwa kutumia mikakati mbalimbali ya utangazaji kama vile vipeperushi; majarida mfano (Afrika Asilia, Selling Tanzania, Tan Travel, Tanzania Explore Magazine na Tanzania Map; tovuti yenye anuani www.tanzaniatourism.com; mitandao mbalimbali ya kijamii mfano youtube, instagram, twitter, facebook; Tanzania Tourism App inayopatikana kwenye Google Play Store kwenye simu za mkononi aina ya smart phone. Vilevile, utangazaji hufanyika kwa kutumia maonesho mbalimbali ndani na nje ya nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara kwa kushirikiana na mikoa na wilaya inaendelea kubaini maeneo ya fukwe katika mwambao wa bahari ya Hindi kwa ajili ya uendelezaji wa shughuli za utalii kama vile kuzamia (scuba diving), kuogelea (swimming), michezo ya kuvua samaki (sport fishing), kupiga mbizi (snorkeling) na sunbathing. Aidha, Serikali inaendelea kutoa elimu kwa wananchi hususan wavuvi ili kuwatunza samaki aina ya papa potwe. Hivi karibuni, Serikali itazindua studio ya utalii, channel ya utalii itakayokuwa chini ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na utambulisho wa Tanzania (Destination Branding). Hatua hii itaongeza ufanisi katika kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini. (Makofi)