Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 11 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 89 2016-05-03

Name

Halima Ali Mohammed

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HALIMA ALI MOHAMMED aliuliza:-
Je, Serikali imefanikiwa kwa kiasi gani kuimarisha majengo na vituo vya Polisi sanjari na kulipa madeni ya Wakandarasi waliojenga majengo hayo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Halima Ali Mohammed, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua uchakavu na uhaba wa majengo ya ofisi za Polisi pamoja na nyumba za makazi kwa Askari. Serikali imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali za kukarabati ofisi na vituo vya Polisi na kujenga nyumba za kuishi Askari. Mathalani, mwaka 2012 Serikali ilijenga maghorofa 15, katika maeneo ya Buyekela Mkoa wa Kagera, matatu yenye uwezo wa kuchukua familia 12. Mkoa wa Mwanza Mabatini sita yenye uwezo wa uchukua familia 24 na Mkoa wa Mara Musoma sita yenye uwezo wa kuchukua familia 24.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa ikiwalipa Wakandarasi wa miradi ya ujenzi wa ofisi na makazi ya Askari kwa awamu kadri ya upatikanaji wa fedha za maendeleo. Mathalani katika mwaka wa fedha wa 2016/2017 Serikali imetenga kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni tano kwa ajili ya maendeleo.