Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 9 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 113 2018-09-14

Name

Muhammed Amour Muhammed

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Bumbwini

Primary Question

MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED aliuliza:-
Kwa kipindi cha kirefu sasa nchi yetu imekuwa ikipeleka Askari wa Jeshi la Wananchi (JWTZ) nje ya nchi ambako kuna vita vya wenyewe kwa wenyewe na kusababisha misiba mikubwa sana kwa Askari wetu:- Je, Serikali inasema nini kuhusiana na kadhia hiyo?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Muhammed Amour Muhammed, Mbunge wa Bumbwini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania kama Mwanachama wa Umoja wa Mataifa, Umoja wa Afrika, Jumuiya za Kikanda kama East Africa Community na SADC na Jumuiya ya Nchi za Maziwa Makuu inao wajibu wa kushiriki katika Ulinzi wa Amani katika nchi mbalimbali. Madhumuni ya kupeleka askari wetu huko ni kwenda kulinda amani na sio kushiriki kwenye mapigano. Kwa bahati mbaya sana, yapo matukio ya kushambuliwa kwa askari wetu yaliyofanywa na vikundi vya waasi yaliyopelekea kupoteza maisha ya baadhi ya askari wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Wananchi wa Tanzania limechukua hatua ya kutoa mafunzo ya kutosha kwa vikosi vyetu vinavyopewa jukumu hili, pamoja na kuwaongezea vifaa vya kisasa ili waweze kujilinda dhidi ya mashambulio ya vikundi vya waasi. Hivyo, mtazamo wa Serikali ni kuendelea kushiriki katika shughuli za Ulinzi wa Amani katika nchi mbalimbali ili kutimiza wajibu wetu Kimataifa na huku tukichukua kila tahadhari kuepusha maafa yaliyowahi kutokea.