Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 9 Energy and Minerals Wizara ya Madini 112 2018-09-14

Name

Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:-
Je, ni lini mgodi utafunguliwa katika eneo la Nyakafuru Wilayani Mbogwe baada ya utafiti kuchukua muda mrefu kwenye eneo hilo?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. DOTO M. BITEKO) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Madini napenda kujibu swali la Mheshimiwa Augustino Manyanda Masele, Mbunge wa Mbogwe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la Nyakafuru lenye leseni ya ukubwa wa kilomita za mraba 17.53 linamilikiwa na Kampuni ya Mabangu Limited Resources, kampuni ambayo Kampuni tanzu ya Resolute Tanzania Limited kupitia leseni ya kutafuta madini PL Na.5374 ya mwaka 2008. Leseni hiyo ambayo ilihuishwa mara mbili na baadaye kuongezewa muda wa kipindi cha miaka miwili yaani extension kuanzia tarehe 24 Oktoba, 2016 ili kukamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na itamaliza muda wake tarehe 23 Oktoba, 2018.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, marekebisho ya Sheria ya Madini ya mwaka 2010 yaliyofanyika mwaka 2017 yaani The Written Laws Miscellaneous Amendment Act 2017 yaliondoa uhitaji wa leseni ya utafutaji wa madini kuongezewa muda wa kufanya utafiti baada ya muda wa leseni kuhuishwa kwa mara ya pili kumalizika. Kwa sasa sehemu ya eneo hilo la leseni hiyo imevamiwa na wachimbaji wadogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi sasa mashapo yanayofikia takribani tani 3.36 yenye dhahabu ya wakia 203,000 yamegunduliwa na jumla ya Dola za Kimarekani milioni 1.83 zimetumika kufanya utafiti katika eneo la mradi. Aidha, Tathmini ya Athari ya Mazingira ilishafanyika na kupewa cheti cha tarehe 16/10/2015.
Mheshimiwa Mwenyekiti, isitoshe, Kampuni ya Mabangu Mining Limited kupitia Kampuni mama ya Resolute (Tanzania) Limited inadaiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania kiasi cha jumla Sh.143,077,421,804 ikiwa ni deni la kodi ambalo wanatakiwa kulilipa. Mgodi wa Nyakafuru unaweza kuendelezwa baada ya deni hilo kuwa limelipwa.