Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 9 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 110 2018-09-14

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:-
Kumekuwa na ucheleweshaji wa mishahara kwa watumishi wa umma:-
Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo hilo?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Waraka wa Hazina Na.12 wa mwaka 2004, watumishi wa umma wanatakiwa kulipwa mishahara yao kabla ya tarehe 25 ya kila mwezi. Kumbukumbu za malipo ya mishahara kwa watumishi wa umma zinaonyesha kuwa, kuanzia Julai, 2017 hadi Agosti, 2018 watumishi walilipwa mishahara yao kati ya tarehe 20 na 24 ya kila mwezi. Hivyo basi, napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu na umma kwa ujumla kuwa hakuna ucheleweshaji wa malipo ya mishahara kwa watumishi wa umma.