Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 72 2018-09-11

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:-
Halmashauri ya Mji wa Tarime imebahatika kuwa na Uwanja wa Ndege wa Magena ambao umekuwa ukitumiwa na watalii wanaokwenda Mbuga ya Serengeti, viongozi mbalimbali na hata Mgodi wa Acacia. Miundombinu ya uwanja pamoja na barabara zake ni mbovu sana.
(a) Je, ni lini Serikali itapanua uwanja huu na kurekebisha miundombinu yake ili ndege nyingi ziweze kutua kwa ajili ya watalii waendao Serengeti?
(b) Je, ni kwa nini Serikali haijajenga jengo la Uhamiaji katika uwanja huo ili kutoa urahisi wa watalii wanaotumia uwanja huo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko, Mbunge wa Tarime Mjini lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kiwanja cha Ndege Magena kinachomilikiwa na Halmashauri ya Mji wa Tarime kina urefu wa mita 1,470 na upana wa mita 120. Kiwanja hicho kimekodishwa kwa mwekezaji ambaye ni Kampuni ya Coastal Aviation kwa mkataba wa kuilipa Halmashauri kiasi cha milioni 20 kila mwaka. Halmashauri imefanya ukarabati wa baadhi ya miundombinu ya kiwanja ikiwemo kujenga barabara yenye urefu wa kilometa 1.2 kutoka barabara ya Tarime – Sirari kwa kiwango cha changarawe ili kuboresha mazingira ya uwanja huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia halmashauri ya Mji wa Tarime ina mpango wa kujenga Ofisi za Uhamiaji ili kuweka utaratibu mzuri wa kuingia na kutoka kwa watalii wanaokwenda hifadhi ya taifa ya Serengeti.