Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 61 2018-09-10

Name

Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA (K.n.y. MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU) aliuliza:-
Gereza la Wilaya ya Igunga linakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo ukosefu wa ngome, hakuna Ofisi za Mkuu wa Gereza na Utawala, hakuna nyumba za askari lakini pia gereza hilo ni dogo na linahudumia wafungwa na mahabusu wa kiume tu, wafungwa na mahabusu wa kike hupelekwa Gereza Wilaya ya Nzega.
Je, ni lini Serikali itajenga Gereza la Wilaya ya Igunga ili liweze kutoa huduma bora kwa wafungwa mahabusu Wilayani Igunga?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dalaly Peter Kafumu, Mbunge wa Igunga, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ujenzi wa gereza la mahabusu Wilaya ya Igunga ulianza mwaka 2003 ili kuwapokea na kuwahifadhi mahabusu na wafungwa kutoka Wilaya ya Igunga ambao walikuwa wakipelekwa na kuhifadhiwa katika Gereza la Nzega ambalo nalo ni dogo na hivyo kusababisha msongamano mkubwa. Ujenzi huo bado haujakamilika kwani unafanyika kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha.
Mheshimiwa Spika, ujenzi wa gereza hilo utakapokamilika kutakuwa na maeneo yote muhimu yanayotakiwa kwenye gereza kama vile ngome, ofisi, mabweni ya wafungwa na mahabusu, jiko, bwalo la chakula na litakuwa na uwezo wa kuhifadhi wafungwa na mahabusu wa jinsia zote.