Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Madini 51 2018-09-07

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA (K.n.y. MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA) aliuliza:-
Katika kutekeleza Mkataba wa Corporate Social Responsibility (CSR), Mgodi wa GGM unatumia bei za manunuzi kutoka nchi ya Afrika Kusini, mfano bei ya bati moja ni shilingi 81,000 na bei ya mfuko wa saruji ni shilingi 48,000.
Je, kwa nini Serikali isiziite pande hizi mbili, Mgodi wa GGM na Halmashauri ili iweze kumaliza mgogoro huo na kuweka utaratibu mzuri?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Madini, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Joseph Kasheku Musukuma, Mbunge wa Geita Vijijini kama lilivyoulizwa na Mheshimiwa Bukwimba, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutekeleza matakwa ya Sheria ya Madini ya mwaka 2010 na marekebisho yake ya mwaka 2017 kifungu cha 105, Halmashauri ya Mji wa Geita na Halmashauri ya Wilaya ya Geita pamoja na Mgodi wa Dhahabu wa GGM zimeandaa Mpango wa Uwajibikaji wa Kampuni kwa Jamii wa mwaka 2018 (Corporate Social Responsibility Plan, 2018).
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuandaa mpango huo uliokuwa shirikishi, GGM iliwasilisha bei ya bati la geji 28 kwa kipimo cha mita za mraba ambapo bei ya mita moja ya mraba ilikuwa ni shilingi 81,000 na bei ya mfuko wa saruji ilikuwa ni shilingi 48,000 kwa mfuko mmoja. Aidha, baada ya bei hizo zilizopendekezwa na mgodi kuonekana kuwa ni kubwa, pande zote mbili ambazo ni Halmashauri ya Mji wa Geita na Halmashauri ya Wilaya ya Geita pamoja na Kampuni ya GGM walikaa na kufanya majadiliano ya pamoja na kukubaliana bei zilizopendekezwa na GGM zirekebishwe kwa kuweka bei ya bati moja na siyo bei ya bati kwa mita za mraba ambapo bati moja geji 28 ilikubalika kuwa shilingi 27,000 na mfuko mmoja wa saruji kuwa shilingi 18,000.