Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 4 Good Governance Ofisi ya Rais TAMISEMI. 41 2018-09-07

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO (K.n.y. MHE. MARYAM SALUM MSABAHA) aliuliza:-
Mradi wa TASAF ni mradi wa kusaidia kaya maskini nchini. Je, ni wananchi wangapi ambao wananufaika na mradi huo katika Visiwa vya Pemba na Unguja?

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maryam Salum Msabaha, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini ulianza rasmi januari 2013. Mpango huu ni wa miaka 10 iliyogawanyika katika vipindi viwili vya miaka mitano mitano na unatekelezwa hadi 2023 katika Halmashauri zote Tanzania Bara na Zanzibar. Jumla ya kaya maskini milioni 1.1 zenye jumla ya watu takribani milioni tano zimeandikishwa katika jumla ya vijiji, mitaa na shehia 9.986.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Zanzibar, Unguja na Pemba kaya zilizonufaika na mpango huu kwa kupatiwa ruzuku na ajira kwa kushiriki kwenye kazi katika miradi ya kutoa ajira ya muda mfupi na vikundi vya kuweka akiba na kuwekeza kwa lengo la kukuza uchumi wa kaya ni 32,262 kutoka katika shehia 168. kati ya idadi hiyo kaya 18,092 ni kutoka Unguja na kaya 14,164 ni kutoka pemba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jumla ya shilingi bilioni 32 zimetumika tangu mpango uanze kama ifuatavyo:-
(a) Miradi ya kutoa ajira za muda shilingi 7,240,498,800;
(b) Ruzuku kwa masharti ya elimu na afya ni shilingi 25,24,002,721; na
(c) Vikundi vya kukuza uchumi wa kaya zilizotolewa ni shilingi 464,000,000.