Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 40 2018-09-07

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-
Kutokana na sera ya Serikali kujenga vituo vya afya kila kata.
Je, ni lini Serikali itajenga vituo hivyo katika Kata za Maretadu, Maghangw, Endamilay, Dinamu, Geterer, Masieda na kupandisha hadhi Zahanati ya Hayderer kuwa Kituo cha Afya?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Gregory Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2017/2018 Serikali imejenga vituo vya afya 210 nchi nzima kwa gharama ya shilingi bilioni 93.5 vikiwemo vituo vya afya saba vilivyoko Mkoa wa Manyara kwa gharama ya shilingi bilioni 3.1ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu ilipewa shilingi milioni 400 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Dongobeshi na Halmashauri ya Miji Mbulu ilipewa shilingi bilioni moja kwa ujenzi wa Vituo vya Afya vya Tlawi na Daudi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutimiza azma ya kuwa na kituo cha afya kila kata hapa nchini Serikali imeweka vigezo maalum juu ya ujenzi wa vituo vya afya, lengo mahsusi ni kusogeza huduma za afya ili zipatikane ndani ya umbali wa kilometa tano kama ilivyoelekeza kwenye Mpango wa Maendeleo wa Afya ya Msingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kupandishwa hadhi kwa Zahanati ya Hayderer kuwa kituo cha afya miundombinu iliyopo katika zahanati hiyo haikidhi vigezo vya kuhuishwa kutoa huduma kama kituo cha afya. Aidha, Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu imeendelea kufanya uhamasishaji kwa wananchi kujitolea kujenga vituo vya afya katika kata zilizotajwa za Maretadu, Maghangw, Endamilay, Dinamu, Geterer na Masieda. Hadi sasa wananchi wa Maretadu wametenga eneo lenye ukubwa wa ekari 10 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa kituo cha afya katika kata hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaunga mkono nguvu za wananchi katika ujenzi kulingana na upatikanaji wa fedha na rasilimali nyingine kama watumishi na vifaa tiba.