Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 19 2018-09-05

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AISHAROSE N. MATEMBE aliuliza:-
Mkoa wa Singida unakua kwa kasi sana na ujenzi wa majengo makubwa ya kisasa umeongezeka, lakini kwa muda mrefu sasa hakuna gari la zimamoto linaloweza kuhudumia mkoa; gari lililopo kwa sasa ni bovu na lina ujazo wa lita 1,500 tu na lenye ujazo wa lita 7,000 lilipata ajali miaka iliyopita na Serikali iliahidi kulifanyia matengenezo lakini mpaka sasa haijafanya hivyo:-
Je, ni lini Serikali itapeleka gari la kisasa la zimamoto Mkoani Singida ili kukabiliana na majanga ya moto yanayoweza kutokea?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Aisharose Matembe, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuwa Mkoa wa Singida unakua kwa kasi ingawa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji lina gari moja lenye ujazo wa lita 1,500 ambalo linafanya kazi zake na gari la pili ni bovu. Hata hivyo, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linatarajia kulifanyia matengenezo gari la pili ambalo ujazo wake ni lita 7,000 na pindi fedha zitakapopatikana gari zote mbili zitaweza kufanya kazi kwa pamoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuimarisha shughuli za zimamoto na uokoaji, Serikali kwa kupitia bajeti ya mwaka 2018/2019, imepanga kununua gari tano za zimamoto ambazo zitagawiwa katika maeneo mbalimbali nchini yenye uhitaji mkubwa. Aidha, Wizara inaandaa marekebisho ya Sheria ya Zimamoto na Uokoaji Namba 14 ya Mwaka 2017 ili kuzitaka halmashauri za manispaa, miji na wilaya kununua magari ya kuzimia moto ili kuondokana na upungufu mkubwa wa magari uliopo hivi sasa.