Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 11 2018-09-04

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. PAULINE P. GEKUL (K.n.y. MHE. JOSEPH M. MKUNDI) aliuliza:-
Je, lini Serikali itapeleka umeme katika Vijiji vya Kakerege na Nkilizya vilivyopo Nansio Ukerewe?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Michael mkundi, Mbunge wa Ukerewe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Kijiji cha Nkilizya kina vitongoji saba (7) na kati ya vitongoji hivyo vitatu (3) vya Magereza, Kenonzo na Lwocho, vilipata umeme mwaka 2005 kupitia utekelezaji wa mradi wa kupeleka umeme Nansio Wilayani Ukerewe kutoka Wilaya ya Bunda ambapo wateja 60 waliunganishiwa umeme. Vitongoji viwili (2) vya Namalebe na Chamatuli vilipatiwa umeme mwaka 2012 kupitia ufadhili wa Benki ya Dunia na jumla ya wateja 47 wameunganishiwa umeme.
Mheshimiwa Spika, vitongoji vingine viwili (2) vya Mumakeke na Bubange vya Kijiji cha Nkilizya visivyokuwa na umeme, pamoja na Kijiji cha Kakerege vitapatiwa umeme kupitia Mradi wa REA III mzunguko wa kwanza unaoendelea kutekelezwa kwa sasa. Kupitia utekelezaji wa mradi huu, jumla ya vijiji 35 katika Wilaya ya Ukerewe vitapatiwa umeme. Kampuni ya Nipo Group Limited aliyepewa kazi za Mradi wa REA III katika Mkoa wa Mwanza anaendelea na utekelezaji mradi huo na mradi unatarajiwa kukamilika Juni, 2019.
Mheshimiwa Spika, kazi za Mradi wa REA III Ukerewe zinajumuisha ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilomita 78.32; njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilomita 156; ufungaji wa transfoma 78 za KVA 50 na 100; pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 2,640. Gharama ya mradi ni shilingi bilioni 9.28.