Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 1 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 10 2018-09-04

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:-
Mwaka 2016 Serikali kupitia Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mheshimiwa William Lukuvi aliahidi kuipatia Wilaya ya Mbulu Baraza la Ardhi la Wilaya:-
• Je, ni lini ahadi hiyo itatekelezwa na hatimaye Wilaya ya Mbulu kuwa na Baraza la Ardhi la Wilaya?
• Je, ni kwa nini Serikali isipime ardhi ya wananchi wa Wilaya ya Mbulu na kuwapatia hati ili kuondoa migogoro ya ardhi?

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zacharia Paul Issaay, Mbunge wa Mbulu Mjini, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Spika, mwishoni mwa Julai, 2018 Wizara kupitia Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma imetangaza nafasi za ajira kwa ajili ya kupata Wenyeviti 20 wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya. Wenyeviti hawa ni kwa ajili ya Mabaraza 17 ambayo hayana Wenyeviti. Vilevile Wenyeviti wawili ni kwa ajili ya kuongeza nguvu kwenye Mabaraza katika Mikoa ambayo imeelemewa na mashauri mengi na ina Mwenyekiti mmoja kama Dar es Salaam na Mwenyekiti mmoja ni kwa ajili ya Baraza la Mbulu ambalo litafunguliwa na kuanza kufanya kazi punde taratibu za kupata watumishi wengine zitakapokamilika. Kwa ushauri wa Mkoa na Wilaya Baraza hili litakuwa Makao Makuu ya Wilaya ya Mbulu.
(b) Mheshimiwa Spika, azma ya Serikali ni kuhakikisha kuwa kila kipande cha ardhi nchini kinapimwa. Azma hii inatekelezwa kwa kupeleka huduma zote za sekta ya ardhi ikiwemo huduma za upimaji katika Ofisi za Ardhi za Kanda na Wapima wa Wilaya. Aidha, Wizara imekalimisha taratibu za kupeleka vifaa vya kisasa ambavyo vitasaidia zoezi hili la upimaji na TEHAMA katika ngazi za Kanda vyenye thamani ya shilingi bilioni 4.3 ambavyo zimekabidhiwa kwa viongozi wa Kanda wiki hii ambavyo vitasaidia sana katika kurahakisha zoezi hili la upimaji katika Wilaya zetu katika Kanda husika.
Mheshimiwa Spika, napenda kukumbusha kuwa jukumu la upimaji ni la Mamlaka ya Upangaji, hivyo, Halmashauri zote zinatakiwa kushirikiana na Wizara kupitia Afisa Ardhi, Ofisi za Ardhi za Kanda, kuhakikisha kuwa azma ya kupima kila kipande cha ardhi nchini inafikiwa.