Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 04 2018-09-04

Name

Sonia Jumaa Magogo

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SONIA J. MAGOGO aliuliza:-
Je, Serikali inasaidiaje watoto wa Shule za Msingi Wilayani Handeni ambao wamekuwa wakisongamana sana kwenye darasa moja?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwanza naomba uniruhusu nimkaribishe Mheshimiwa Sonia kwenye kazi za Bunge baada ya kuwa ameugua kwa muda mrefu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sonia Jumaa Magogo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ongezeko la wanafunzi katika shule za msingi na sekondari ni moja ya changamoto iliyotokana na utekelezaji wa Sera ya Elimu Bila Malipo. Katika mwaka wa fedha 2016/2017, Serikali ilikamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa sita kwa kiasi cha shilingi milioni 40.96 katika shule za msingi Kwazala, Ugweno na Gumba na Mbunge wa Handeni Mheshimiwa Mboni Mhita, kupitia fedha za Mfuko wa Jimbo alikamilisha ujenzi wa madarasa saba kwa gharama ya shilingi milioni 37.63 katika shule za Kabuku Mjini, Gole, Mnyuzi na Msilwa.
Mheshimiwa Spika, vilevile katika mwaka wa fedha 2017/2018, Serikali imejenga vyumba sita vya madarasa kwa gharama ya shilingi milioni 120 katika Shule za Mhalango, Kitumbi na Komkonga na kukamilisha ujenzi wa vyumba sita vya madarasa kwa gharama ya shilingi milioni 23.5 katika Shule za Kwachaga na Kibundu. Aidha, katika mwaka wa fedha 2018/2019, Serikali imetenga kiasi cha shilingi milioni 137.2 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba sita vya madarasa na matundu 12 ya vyoo katika Shule za Msingi Kiselya na Mhalango.
Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kujenga miundombinu ya elimu katika Halmashauri ya Handeni na inawaomba wananchi na wadau kushiriki kikamilifu katika juhudi za kupunguza tatizo la uhaba wa vyumba vya madarasa, maana Serikali peke yake haitoweza kuwa na bajeti ya kutosheleza mahitaji yote ya Ujenzi wa miundombinu ya shule kwa kipindi kifupi.