Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 03 2018-09-04

Name

Livingstone Joseph Lusinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtera

Primary Question

MHE. OMARY A. BADWEL (K.n.y. MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE) aliuliza:-
Je, ni lini barabara ya kutoka Mpunguzi kupitia Nagula, Mpwajungu, Ituzi hadi Ilangali itapandishwa hadhi kuwa ya Mkoa ambayo itasimamiwa na Mkoa kwa maana ya TANROADS?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Livingstone Joseph Lusinde, Mbunge wa Jimbo la Mtera, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, barabara ya Mpunguzi – Ilangali yenye urefu wa kilometa 88.3 ni barabara mjazo yenye tabaka la changarawe na udongo, ambayo inaunganisha Wilaya ya Dodoma, Bahi, Chamwino na kwa upande mwingine inaunganisha Mkoa wa Dodoma na Mkoa wa Iringa, Wilaya ya Iringa Vijijini. Upande wa Dodoma Jiji ina kilometa tatu, Bahi kilometa 18.3 na Chamwino kilometa 67.
Mheshimiwa Spika, kwa kutambua umuhimu wa barabara hii, Serikali ilitengeneza sehemu ya Mpunguzi hadi Nagulo kwa kiwango cha changarawe yenye urefu wa kilometa 21.3 kwa gharama ya shilingi bilioni 3.032 katika mwaka wa fedha 2015/2016 kwa ufadhili wa DFID. Aidha, barabara ya Mpunguzi – Ilangali katika mwaka wa fedha 2017/2018, Serikali kupitia TARURA iliifanyia matengenezo ya sehemu korofi kwa urefu wa kilometa 17 yaliyogharimu shilingi milioni 86.2 na katika mwaka wa fedha 2018/2019, TARURA Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino imetenga shilingi milioni 170 za kuifanyia matengenezo ya muda maalumu kwa urefu wa kilometa 8.5 na kazi hii ipo katika hatua za manunuzi.
Mheshimiwa Spika, maombi ya kupandishwa hadhi barabara ya Mpunguzi – Ilangali kwa sasa yapo ngazi ya Mkoa. Pindi yatakapowasilishwa kwa Waziri mwenye dhamana na kuonekana kwamba yanakidhi vigezo vilivyowekwa na sheria, barabara hii itapandishwa hadhi.