Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 34 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 293 2018-05-22

Name

Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:-
Je, Idara ya Mahakama iliandika Ripoti za Sheria (Law Reports) ngapi kwa mwaka 2017?

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Tanzania inatumia mfumo wa kisheria wa Common Law ambao maamuzi ya Mahakama za juu yana nguvu ya kisheria na yanazibana Mahakama nyingine za chini katika kufanya maamuzi ya kesi. Msingi huo wa kisheria unaofahamika stare decisis unazitaka Mahakama kutumia misingi ya tafsiri ya kisheria yaliyotolewa na Mahakama za juu na wakati mwingine zilizoamuliwa na Mahakama iliyo na mamlaka sawa endapo kesi zinafanana. Hata hivyo, Mahakama ya juu kabisa kama ilivyo Mahakama ya Rufani hapa Tanzania inaweza na ina mamlaka ya kubadilisha msingi au tafsiri ya sheria iliyotajwa huko nyuma inaposikiliza shauri jipya.
Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha msingi huo unafuatwa, uchapishaji wa mara kwa mara wa maamuzi ya Mahakama katika Law Reports ni muhimu ili wanasheria, Majaji na watu wote waweze kujua ni msingi gani na uamuzi upi wa sheria umewekwa na Mahakama katika kesi fulani iliyofikishwa Mahakamani na kuamuliwa. Kwa kufuata utaratibu huo, tangu mwaka 1921 Law Reports zimekuwa zikichapishwa Tanzania. Hivyo basi, taarifa za sheria ni mfululizo wa vitabu ambavyo vina maoni ya Mahakama kutoka kwenye baadhi ya kesi zilizoamuliwa na Mahakama ambazo zinatakiwa kufuatwa na Mahakama nyingine.
Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2017 Mahakama ya Tanzania kupitia Bodi ya Uhariri ya Taarifa za Sheria za Tanzania (Tanzania Law Reports Editorial Board) imeandaa Law Reports zipatazo nne ambazo ni Law Report ya mwaka 2014, 2015, 2016 na 2017. Kwa sasa Law Reports hizo zipo katika hatua na taratibu za mwisho ikiwa ni pamoja na kufanyiwa uhakiki wa kina wa kiuhariri na taratibu zingine za ununuzi kwa ajili ya kumpata mzabuni wa kuchapisha Law Reports rasmi.