Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 32 Good Governance Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 270 2018-05-18

Name

Prosper Joseph Mbena

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. PROSPER J. MBENA aliuliza:-
Nchi nyingi duniani ikiwemo Japan, Uholanzi na Marekani hutumia wataalam wastaafu kwenye sekta mbalimbali za uchumi katika shughuli mbalimbali za kutoa ushauri ndani na nje ya nchi zao. Wataalam hao (volunteers) wanatoa mchango mkubwa kwenye kushauri.
(a) Je, ni lini nchi yetu itaiga utaratibu huo mzuri wa kuwatumia wataalam wake wastaafu ipasavyo badala ya kuwaacha tu mitaani?
(b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuweka kumbukumbu ya taarifa ya wataalam wastaafu wake (directory) kwa kila mmoja kwenye fani yake (profession) ili kuweza kuwatumia wataalam wastaafu hao pale ushauri wao utakapohitajika?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA MADINI (K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI UMMA NA UTAWALA BORA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Prosper Joseph Mbena, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Spika, Serikali inao utaratibu wa kuwatumia wataalam wastaafu kwa kuwapatia mikataba pale wanapohitajika. Matumizi ya wataalam hao yamefanunuliwa katika aya ya 12.2 ya Waraka wa Rais Namba 1 wa mwaka 1998, pamoja na Kanuni ya D. 28 ya Kanuni za Kudumu (Standing Orders) katika Utumishi wa Umma za mwaka 2009. Miongozo hii inaelekeza kwamba endapo utaalam wa mtumishi unahitajika sana Serikali inawajibika kumuomba mtumishi kuendelea na kufanya kazi.
(b) Mheshimiwa Spika, Serikali inapokea ushauri wa Mheshimiwa Mbunge wa kuanzisha kanzidata ya wataalam wastaafu ili kuweza kuwatumia pale watakapohitajika.