Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 30 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 251 2018-05-16

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza:-
Wabunge wa Viti Maalum ni sawa na Wabunge wengine wa Majimbo kwa sababu hakuna tofauti ya kiapo cha Wabunge wa Majimbo na wale wa Viti Maalum.
Je, ni kwa nini Wabunge wa Viti Maalum hawaingii kwenye Vikao vya Kamati ya Fedha za Halmashauri zao?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Taska Restituta Mbogo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango, imeundwa kwa mujibu wa Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) Sura ya 287, kifungu cha 75 na Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji), Sura ya 288 kifungu cha 47 pamoja na kifungu cha 40(2)(c) cha Kanuni za Kudumu za Halmashauri za mwaka 2014 na Kanuni za Kudumu za Mamlaka za Serikali za Mitaa kifungu 41(1) zinazotaja Wajumbe wa kuingia kwenye Kamati ya Fedha na Mipango kuwa ni Meya au Mwenyekiti wa Halmashauri ambaye atakuwa Mwenyekiti; Naibu Meya au Makamu Mwenyekiti, Mbunge au Wabunge wa Majimbo wanaowakilisha Majimbo katika Halmashauri hiyo; Wenyeviti wa Kamati za Kudumu katika Halmashauri; Wajumbe wengine wasiozidi wawili watakaopendekezwa na Mwenyekiti au Meya na kupigiwa kura na Baraza la Madiwani la Halmashauri, mmoja kati yao akiwa mwanamke.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wabunge wa Viti Maalum hawaingii kwenye vikao vya Kamati za Fedha za Halmashauri kwa sababu hawajatajwa kwenye orodha ya Wajumbe iliyoainishwa na kifungu cha 41(1) na kifungu cha 40(2) cha Kanuni za Kudumu za Mamlaka za Serikali za Mitaa za Mwaka 2014, zinazofafanua mahitaji ya Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) Sura ya 287, kifungu cha 75 na Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) Sura ya 288 kifungu cha 47.