Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 28 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 231 2018-05-14

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza:-
Mwaka wa 2014/2015, Jimbo la Magu halikupatiwa Walimu wa shule za msingi na bado kuna uhaba wa Walimu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta Walimu Magu?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Boniventura Desderius Kiswaga, Mbunge wa Magu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Magu inao Walimu wa shule za msingi 1,281 kati ya Walimu 2,002 wanaohitajika, hivyo kuna upungufu wa Walimu 821. Kati ya Walimu 1,276 wa shule za msingi walioajiriwa mwezi Disemba, 2017, Halmashauri ya Wilaya ya Magu ilipangiwa Walimu 56 ambao wameripoti kwenye shule zilizokuwa na uhitaji mkubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Walimu 77 ambao ni miongoni mwa Walimu wa ziada wa masomo ya sanaa katika shule za sekondari za Halmashauri ya Wilaya ya Magu wamehamishiwa shule za msingi. Vile vile katika Mwaka wa Fedha 2017/2018, Serikali imepanga kuajiri Walimu 10,130 wa shule za msingi nchi nzima ili kukabiliana na uhaba wa Walimu katika maeneo mbalimbali; na Halmashauri ya Magu nayo itapangiwa Walimu hao. (Makofi)