Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 27 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 227 2018-05-11

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:-
Liwale ni Wilaya ya zamani hapa nchini lakini hadi leo haina jengo la Mahakama zaidi ya jengo lililorithiwa toka iliyokuwa Mahakama ya Mwanzo Liwale.
Je, ni lini Serikali itajenga jengo la Mahakama Liwale sambamba na nyumba za watumishi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zuberi Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakiri kwamba ni kweli Wilaya ya Liwale haina jengo la Mahakama ya Wilaya. Aidha, kama alivyoainisha Mheshimiwa Mbunge ni kweli jengo la Mahakama ya Mwanzo ya Liwale Mjini ambalo linatumika sana kutolea huduma za Mahakama ya Wilaya na ya Mwanzo ni chakavu na hivyo kuhitaji kujengwa upya. Katika mpango wa ujenzi, tumepanga kujenga kujenga Mahakama ya Wilaya ya Liwale kwa mwaka wa fedha 2019/2020 ambalo pia litatumika na Mahakama ya Mwanzo Liwale Mjini, sambamba na ujenzi wa nyumba ya Hakimu kutegemea upatikanaji wa fedha.