Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 26 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 217 2018-05-10

Name

Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINABU M. AMIRI aliuliza:-
Je ni lini Serikali itapunguza bei ya gesi kwa matumizi ya majumbani ili kuwawezesha wananchi wengi zaidi kutumia gesi kwa matumizi yao ya nyumbani na kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zainabu Mndolwa Amiri, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, gesi iliyogunduliwa nchini ni gesi asilia (natural gas) ambayo husafirishwa kutoka kwenye visima vya gesi hadi kwa watumiaji kupitia mabomba. Mpaka sasa watumiaji wakubwa wa gesi hapa nchini ni viwanda na mitambo ya kufua umeme. Mradi wa majaribio wa gesi asilia kwa ajili ya matumizi ya nyumbani ulianza kupitia mradi wa mfano (pilot project) ambapo nyumba 70 zilizopo Mikocheni Jijini Dar es Salaam zimeunganishwa na gesi kwa matumizi ya nyumbani.
Mheshimiwa Spika, hivi sasa gesi inayotumiwa na wananchi kupikia majumbani ni Liquefied Petroleum Gas (LPG) ambayo huagizwa na wafanyabiashara kutoka nje kama ilivyo katika mafuta ya petrol, diesel na mafuta ya taa au ndege. Gesi hii hujazwa katika mitungi kwa ujazo tofauti tofauti na gharama ya gesi hii inategemeana na soko la dunia.
Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuhamasisha wawekezaji katika sekta ya gesi kwa ajili ya matumizi ya majumbani ili kuleta ushindani katika sekta hii. Mpaka sasa makampuni mengi yameanza kujenga miundombinu ya gesi katika sehemu mbalimbali za nchi na kuonesha nia ya kushirikiana na Serikali katika kusambaza gesi asilia nchini.
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TPDC imeanza matayarisho ya kutekeleza mradi wa kuunganisha gesi majumbani ambapo awamu ya kwanza ya mradi huo utapita katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam na Mtwara na baadaye katika mikoa mingine ya nchi yetu. Mheshimiwa Spika, ahsante.