Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 17 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 143 2018-04-25

Name

Yussuf Haji Khamis

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Nungwi

Primary Question

MHE. YUSSUF HAJI KHAMIS aliuliza:-
Kituo cha Polisi cha Mkokotoni kiliungua mnamo tarehe 27/12/2010 na ujenzi wake ulianza mara moja.
Je, ni lini ujenzi huu utakamilika na kituo hicho kuendelea na shughuli zake?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Yussuf Haji Khamis, Mbunge wa Nungwi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuwa kituo cha polisi cha Mkokotoni kilipata ajali ya moto mwaka 2010. Baada ya kuungua kwa kituo hichi, wananchi wa eneo husika waliendelea kupata huduma za kipolisi kupitia jingo lililokuwa pembeni na kituo kilichoungua moto. Serikali kupitia Jeshi la Polisi ilitafuta mkandarasi ambaye alianza kujenga upya kituo hicho na kwa sasa ujenzi wake umekamilika kwa asilimia 80. Aidha, shughuli za Kituo cha Polisi cha Mkokotoni zitaanza katika jengo jipya baada ya kukamilika kwa ujenzi wake.