Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 15 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 118 2018-04-23

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:-
Jimbo la Segerea ni moja kati ya Majimbo ya Dar es Salaam ambalo wakazi wake ni wengi na wa kipato cha chini na sababu kubwa ikiwa ni ubovu wa miundombinu ya barabara hasa madaraja na mitaro, hivyo kusababisha mafuriko ya mara kwa mara.
Je, ni lini Serikali itajenga madaraja ya Tabata Kisiwani na Kisukuru sambamba na kujenga mitaro ili kupunguza adha ya mafuriko katika Kata za Jimbo hili?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anatropia Lwehikila Theonest, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuhudumia wananchi wa Jimbo la Segerea katika kuboresha na kufanya matengenezo ya miundombinu ya barabara, madaraja pamoja na mitaro.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutatua tatizo la adha ya mafuriko yanayotokana na mvua maeneo ya Tabata, Halmshauri ya Manispaa ya Ilala kupitia mradi wa DMDP imepanga kujenga mifereji ya maji ya mvua yenye urefu wa kilometa 9.82 na vivuko katika bonde la Msimbazi – Tenge – Lwiti – Sungura na Tembomgwaza kwa gharama ya shilingi bilioni 15 ambazo zabuni za ujenzi huo zinatangazwa mwezi Mei, 2018. Hivyo, baada ya ujenzi wa mifereji hiyo na vivuko, tatizo la mafuriko kwa wananchi wa Tabata Kisiwani na Kisukuru litapungua. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Mawenzi - Tabata - Kisiwani kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilitengewa shilingi milioni 180 za kufanyia matengenezo kwa kiwango cha Changarawe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, katika mwaka wa fedha 2018/2019, Manispaa ya Ilala imeyenga shilingi milioni 40 za kuifanyia matengenezo ya kawaida na kukarabati daraja lililopo eneo la Mwananchi.