Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 14 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 114 2018-04-20

Name

Njalu Daudi Silanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Itilima

Primary Question

MHE. NJALU D. SILANGA aliuliza:-
Shirika la Nyumba lilianzishwa kwa ajili ya kusaidia watumishi wa umma pamoja na wananchi wenye maisha ya chini na Mkoa wa Simiyu ni mpya ambapo tayari kuna watumishi wengi ambao hawana nyumba za kuishi ikiwemo Wilaya za Itilima na Busega:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba katika Mkoa mpya wa Simiyu pamoja na wilaya zake kwa kutumia Shirika la Nyumba?

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Njalu Daudi Silanga, Mbunge wa Itilima, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Shirika la Nyumba la Taifa lilipokea maombi ya ujenzi wa nyumba kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Itilima mwaka 2014. Baada ya kupokea maombi hayo shirika liliendelea na hatua nyingine za maandalizi ikiwa ni pamoja na kuandaa mpango wa kina wa matumizi ya ardhi, kuandaa michoro ya nyumba na kukadiria gharama za nyumba husika.
Mheshimiwa Naibu Spika, Shirika liliingia makubaliano na Halmashauri ya Wilaya ya Itilima ya kujenga jumla ya nyumba 14 tarehe 2 Julai, 2005. Kati ya nyumba hizo 13 za Wakuu wa Idara na moja ni ya Mkurugenzi wa halmashauri. Utekelezaji mradi huu ulipangwa kuanza mara moja baada ya halmashauri kulipa kiasi cha shilingi bilioni 400 ikiwa ni awamu ya kwanza ya malipo ya nyumba husika. Hata hivyo, Halmashauri ya Itilima haijafanya malipo hayo hadi sasa na hivyo kuchelewesha kuanza kwa mrai huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuzipongeza Halmashauri za Momba, Busekelo, Mlele, Mvomero, Monduli, Uyui, Kongwa na Geita na nyingine kwa ushirikiano ambao umewezesha watumishi wao kujengewa nyumba na Shirika la Nyumba la Taifa. Natoa wito kwa halmashauri zote uhitaji wa nyumba kuwasilisha maombi ya kujengewa nyumba na Shirika la Nyumba ili maombi hayo yaweze kufanyiwa kazi na kuwapatia makadirio ya gharama za ujenzi ili kazi hiyo iweze kufanywa na Shirika la Nyumba.