Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 10 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 73 2016-05-02

Name

Kemirembe Rose Julius Lwota

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KEMIREMBE J. LWOTA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itapeleka x-ray na CT-Scan kwenye Hospitali ya Sekou Toure Mkoani Mwanza?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kemirembe Julius Lwota, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali ya Mkoa wa Mwanza ya Sekou Toure ina mashine mbili za x-ray ambazo zilinunuliwa na Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto mwaka 2002. X-Ray hizo zinafanya kazi pamoja na kuwepo kwa matengenezo ya mara kwa mara kutokana na uchakavu wake. Aidha, hospitali hiyo haina mashine ya CT-Scan na kwamba huduma hiyo inapatikana katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wizara ya Afya imeanza mradi wa kusimika vifaa vya kuangalia mwenendo wa afya za wagonjwa na vifaa vya uchunguzi vikiwemo CT-Scan katika Hospitali za Rufaa za Mikoa utakaotekelezwa kwa ushirikiano wa Serikali ya Tanzania na Uholanzi. Mpango huu utakapokamilika utasaidia Hospitali nyingi za Mikoa za Rufaa kuwa na vifaa muhimu kwa ajili ya huduma ya afya.