Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 65 2018-04-12

Name

Saul Henry Amon

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. SAUL H. AMON aliuliza:-
Barabara ya Pakati – Njugilo – Masukulu – Matwebe hadi mpakani ni barabara kubwa na inapita katika Kata nne ambazo ni Masoko, Bujela, Masukulu na Matwebe, barabara hii ilishapandishwa daraja na kuwa ya TANROADS:-
Je, ni lini barabara hii itaanza kujengwa ili kuondoa adha kwa wananchi kwa kupoteza kipato kwa mazao kuharibika njiani?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Saul Henry Amon, Mbunge wa Jimbo la Rungwe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, barabara ya Pakati – Njugilo – Masukulu hadi Mpakani mwa Wilaya ya Rungwe na Kyela yenye urefu wa kilometa 24.5 ni barabara ya wilaya. Katika kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa Muhtasari Na.2016/2017/ 01 cha tarehe 6/12/2016, kilipendekeza ipandishwe hadhi na kuwa barabara ya mkoa. Baada ya mapendekezo kupelekwa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, barabara hiyo iliidhinishwa na kupandishwa hadhi kwa urefu wa kilometa 4.4 kutoka Njugilo hadi Masukulu katika Wilaya ya Kyela.
Mheshimiwa Spika, matengenezo ya barabara hii yanatarajia kuanza Agosti 2018, kufuatia kuwekwa kwenye Mpango wa Uboreshaji wa Miundombinu ya Barabara za Vijijini kupitia ufadhili wa watu wa Marekani (USAID), chini ya programu ya Irrigation and Rural Roads Infrastructure Project – IRRIP II ambapo kwa sasa zipo kwenye hatua ya usanifu.