Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 53 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 439 2017-06-22

Name

Vedasto Edgar Ngombale Mwiru

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA (K.n.y. MHE. VEDASTO E. NGOMBALE) aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuitangaza Wilaya ya Kilwa kuwa ni moja ya maeneo makubwa ya Kiutalii katika Kanda ya Kusini kwa kuzingatia historia yake, maajabu mbalimbali yaliyopo, fukwe, mapango, malikale, mbuga, mabwawa na utamaduni wake?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Vedasto Edger Ngombale, Mbunge wa Kilwa Kaskazini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, nakubaliana na hoja ya Mheshimiwa Mbunge kuwa Wilaya ya Kilwa ni miongoni mwa maeneo yenye fursa za uendelezaji utalii wa kihistoria na kiutamaduni yakiwemo magofu ya malikale yaliyopo eneo la Kilwa Kisiwani na Songo Mnara ambayo ni maeneo yaliyopo kwenye orodha ya urithi wa dunia pamoja na vivutio vingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuitangaza Wilaya ya Kilwa kuwa eneo muhimu la kiutalii Ukanda wa Kusini, Wizara imeandaa jarida la Karibu Kilwa (Kilwa District Heritage Resources); vipeperushi kama Welcome to Kilwa in Tanzania; ambavyo vinaonyesha picha na maelezo ya vivutio vya utalii vilivyopo Wilayani Kilwa na kuanzisha Kituo cha Taarifa za Kiutalii (Tourist Information Centre).
Mheshimiwa Naibu Spika, Jarida na vipeperushi hivi vinatolewa kwa wageni wanaotembelea Kilwa pamoja na kutumika kutangaza utalii wa Kilwa katika maonesho ya
ndani, hususan maonyesho ya Saba Saba; Nane Nane na Maonyesho ya nje ya nchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Wizara kupitia Bodi ya Utalii na kwa kushirikiana na taasisi ya nchini Ufaransa imeweza kuandaa filamu maalumu ambayo inaitangaza Kilwa. Filamu hiyo ilizinduliwa rasmi mwaka 2016 na imetafsiriwa kwa lugha tatu za Kimataifa ambazo ni Kiswahili, Kiingereza na Kifaransa. Filamu hiyo inapatikana kupitia mtandao, kwenye tovuti ya Bodi ya Utalii na kwenye wavuti ya YouTube.