Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 52 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 430 2017-06-21

Name

Dr. Immaculate Sware Semesi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI aliuliza:-
Kwa kuwa Serikali kupitia Idara ya Misitu ina jukumu la kutathmini rasilimali zake ikiwemo miti:-
• Je, Wizara inatekeleza kwa kiwango gani katika kufanya tathmini za idara zake kuangalia athari za magonjwa ya miti?
• Je, nchi inazo ekari ngapi za mioto ya asili na iliyopandwa?
• Je, hadi sasa ni ekari ngapi za miti zimekatwa kwa ajili ya mbao na mkaa?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Immaculate Sware Semesi, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a), (b) na (c), kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Sheria ya Misitu Namba 14 ya Mwaka 2002, shughuli zote za utafiti za kitaalam kuhusiana na magonjwa ya miti na athari zake hutekelezwa na Taasisi ya Utafiti wa Misitu (TAFORI) chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Taasisi hii hufanya utafiti wa utambuzi wa aina ya magonjwa, ukubwa wa matatizo na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukua kutegemeana na uzito wa matokeo ya utafiti husika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa ya Tathmini ya Rasilimali Misitu (NAFORMA) iliyotolewa mwaka 2015 inaonesha kuwa nchi yetu ina misitu yenye hekta milioni 48.1 ambapo misitu ya asili ni hekta 47.528, sawa na asilimia 98.8 na misitu ya kupandwa ni hekta 572,000, sawa na asilimia tu.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kasi ya uharibifu wa misitu ni kubwa sana bila kujali aina ya uharibifu wa misitu ambapo kiasi cha ekari 372,000 za misitu huangamizwa kila mwaka nchini. Aidha, takwimu zinaonesha kwamba ili kurejesha hali ya misitu nchini katika viwango vyake vya kawaida, kiasi cha jumla ya ekari 185,000, sawa na jumla ya miti milioni 230 kinahitajika kupandwa kila mwaka kwa kipindi cha miaka 17.