Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 52 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 429 2017-06-21

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:-
Ujenzi wa Vituo vya Afya Kata za Mninga na Mtwango bado haujakamilika, hivyo wananchi wa Kata hizo wanaendelea kupata shida ya matibabu:-
Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa vituo hivyo ili wananchi waweze kupata huduma za matibabu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mendrad Lutengano Kigola, Mbunge wa Mufindi Kusini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Mtwango ulianza mwaka 2012, ambapo umeshagharimu Sh.22,500,000/=. Aidha, Kituo cha Afya Mninga kilianza kujengwa mwaka 2008 ambapo umegharimu Sh.41,000,000/=. Vituo hivyo vipo katika hatua ya umaliziaji wa majengo ya OPD na nyumba za watumishi ili huduma zianze kutolewa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka wa fedha wa 2016/2017, Serikali ilitenga Sh.32,500,000 kwa ajili ya kuendelea kuchangia ukamilishaji wa Vituo vya Afya Kata ya Mninga na Mtwango. Fedha zilizopokelewa mpaka sasa ni Sh.8,000,000/=. Aidha, katika mwaka wa fedha 2017/2018, zimetengwa Sh.65,000,000/= kwa ajili ya kuimarisha Vituo vya Kasanga na Kituo cha Afya Mbalamaziwa katika Jimbo la Mufindi Kusini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni mpango wa Serikali kuunga mkono juhudi za wananchi katika miradi ya maendeleo kwa kutenga fedha kupitia LGDG kila mwaka ili kumalizia miradi mbalimbali.