Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 50 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 411 2017-06-19

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE: RASHID A. SHANGAZI aliuliza:-
Tanzania imeridhia na kuingia mikataba mbalimbali ya kimataifa ikiwemo diplomasia na mahusiano.
Je, ni nchi ngapi na zipi ambazo Watanzania wanaweza kuzitembelea moja kwa moja kwa utaratibu wa visa on entry wakati wa kuingia ukiondoa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Abdallah Shangazi, Mbunge wa Mlalo kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa maelezo kwa kuwa visa ni ruhusa inayoambatana na masharti ambayo hutolewa na nchi husika ili kuwaruhusu raia wa kigeni kuingia, kuondoka au kuwepo nchini katika muda maalum. Ruhusa hiyo inapotolewa katika vituo vya kuingilia nchini inajulikana kama visa on arrival.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu wa utoaji visa on arrival uko katika sura ya makubaliano ama mikataba baina ya nchi na nchi au taratibu zinazotokana na matengamano na ushirikiano wa kimataifa na kikanda. Utaratibu huu unaweza kubadilika kulingana na mahusianao na hali ya usalama kati ya nchi na nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, zipo nchi 16 ambazo Watanzania wanaweza kuzitembelea katika utaratibu wa visa on arrival. Nchi hizo ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Cote d’voire, Djibout, Gabon, Gambia, Ghana, Guinea, Guinea – Bessau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone huu wa visa on arrival, pia zipo nchi 67 duniani ambazo Watanzania wanaweza kuzitembelea bila hitajio la visa.