Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 49 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 403 2017-06-16

Name

Haji Khatib Kai

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Micheweni

Primary Question

MHE. HAJI KHATIB KAI aliuliza:-
Serikali imeandaa utaratibu wa kuliwezesha Jeshi la Wananchi wa Tanzania kufanya shughuli zake kwa kuwapatia posho mbalimbali ikiwemo ration allowance.
Je, ni lini Serikali itaongeza posho hiyo iendane na maisha yalivyo sasa?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Haji Khatib Kai, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Serikali inao utaratibu wa kuliwezesha Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kufanya shughuli zake kwa kuwapatia maafisa na askari posho za aina mbalimbali ikiwemo ration allowance. Serikali imekuwa ikiboresha maslahi na stahiki mbalimbali kwa maafisa na askari kwa kuzingatia hali ya maisha ya wakati husika na uwezo wa Serikali kifedha kumudu kulipa stahiki hizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ration allowance inalipwa kwa maafisa na askari wote. Serikali ilipandisha kiwango cha posho ya chakula (ration allowance) kwa nyakati tofauti. Kwa mfano, mwaka 2011 ration allowance ilikuwa shilingi 7,500, mwaka 2014 ration allowance ilipanda kufikia shilingi 8,500 na mwaka 2015 ilipandishwa kufikia shilingi 10,000, kiasi ambacho kinaendelea kutolewa hadi hivi sasa. Kwa hivyo, Serikali itaendelea kuboresha posho ya chakula na posho nyinginezo kadri uwezo wa Serikali utakavyoruhusu.