Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 65 2016-04-29

Name

Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SILAFU J. MAUFI aliuliza:-
Serikali imeamua kutoa elimu ya kompyuta kwenye shule za sekondari nchini lakini vifaa vya kufundishia havitoshelezi na hata Walimu ni wachache katika maeneo mengi ikiwemo Mkoa wa Rukwa, ambapo ni shule mbili pekee za Mazwi na Kizwite Sekondari ambazo zimeshaanzishwa:-
Je, Serikali ina mpango mkakati upi wa kufanikisha ufundishaji wa somo hilo kwa tija?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Silafu Jumbe Maufi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, utoaji wa elimu ya kompyuta mashuleni umeanza kufanyika kwa baadhi ya shule zenye mazingira yanayowezesha somo hilo kufundishwa. Changamoto zilizopo ni uhaba wa Walimu, ukosefu wa umeme hususani maeneo ya vijijini na uhaba wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia. Serikali inakabaliana na changamoto hizo kwa kupeleka umeme vijijini kupitia Wakala wa Umeme Vijijini (REA), pamoja na kuhakikisha somo la Kompyuta linafundishwa katika Vyuo vya Ualimu ili kuwaandaa walimu watakaofundisha somo hilo mashuleni. Kuhusu upatikanaji wa vifaa mashuleni Serikali inashirikiana na Kampuni ya Microsoft ambayo imeonesha nia ya kuwezesha upatikanaji wa vifaa hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa muda mrefu wa Serikali ni kuimarisha matumizi ya TEHAMA katika ufundishaji mashuleni hususani masomo ya sayansi. Kwa msaada wa Kampuni ya Microsoft imeanza utekelezaji wa mpango huu kwa shule 50 katika Mikoa 25. Kwa Mkoa wa Rukwa shule zilizochaguliwa ni shule ya Sekondari ya Kizwite na Mazwi. Shule hizi mbili kila Mkoa ni vituo vya mafunzo kwa Walimu ili kuwajengea uwezo wa kufundisha kwa kutumia TEHAMA. Kituo cha Mazwi kinaanza kufanya kazi kuanzia Julai, 2016 ambapo kitapewa vifaa vyote muhimu vitavyohitajika katika mafunzo hayo.