Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 43 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 357 2017-06-07

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA (K.n.y MHE. ORAN NJEZA) aliuliza:-
Wananchi wa Jimbo la Mbeya Vijijini wanaipongeza Serikali kwa kuanzisha Wilaya ya Kipolisi Mbalizi.
• Je, ni lini Ofisi ya Wilaya ya Kipolisi ya Mbalizi itajengwa zikiwemo nyumba za kuishi askari?
• Je, Wilaya ya Kipolisi ya Mbalizi ina magari mangapi na Serikali ina mpango gani wa kuboresha miundombinu ya vituo vya polisi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Oran Manase Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijijini, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua ukosefu wa Kituo cha Polisi chenye hadhi ya Wilaya na ukosefu wa nyumba za kuishi askari Wilaya ya Kipolisi Mbalizi. Ni lengo la Serikali kukamilisha ujenzi wa vituo vya polisi kwenye wilaya 65 zilizosalia na ujenzi wa nyumba za makazi. Ujenzi huu utatekelezwa kwa awamu kutegemeana na upatikanaji wa fedha zitakazotengwa katika bajeti kila mwaka na kutumia rasilimali zilizopo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kipolisi ya Mbalizi ina magari mawili, moja liko Mbalizi na lingine lipo kituo kidogo cha Inyara. Serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya Vituo vya Polisi katika Halmashauri ya Mbeya na kwingineko kadri ya upatikanaji wa fedha utakavyoongezeka.