Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 43 Energy and Minerals Wizara ya Madini 352 2017-06-07

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:-
Mji wa Ruangwa Mkoani Lindi una madini mengi lakini wachimbaji walio wengi wa madini hayo ni wachimbaji wadogo wadogo ambao hawana zana za kisasa za kuchimba madini.
Je, Serikali haioni haja ya kuwasaidia kwa kuwapa mikopo ili waweze kununua zana za kisasa za uchimbaji?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hamida Mohamed Abdallah, Mbunge wa Viti Maalaum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini imeweka vipaumbele vya kusaidia wachimbaji wadogo ili kufanya shughuli zao za uchimbaji huo kuwa wa manufaa kwao pamoja na kuongeza pato la Taifa. Vipaumbele hivyo ni pamoja na kuboresha sekta ya uchimbaji madini mdogo kwa kutoa ruzuku kwa wachimbaji hao wadogo ili waweze kuboresha shughuli zao kuwa za kisasa na kuboresha uchenjuaji na shughuli nyingine za uchimbaji. Lakini vipaumbele vingine ni kuwapa ushauri wa kitaalamu, taarifa za upatikanaji wa vifaa vya uchimbaji, mafunzo kwa vitendo pamoja na masoko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kati ya mwaka 2010 na 2013 Serikali ilitoa mikopo ya jumla ya shilingi milioni 910.195 kwa kampuni nane za wachimbaji wadogo. Aidha, kati ya mwaka 2013 na 2015 Serikali ilitoa ruzuku ya shilingi bilioni
• kwa wachimbaji 115 kwa ajili ya uchimbaji wao nchi nzima pamoja na Mkoa wa Lindi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilianza kutoa ruzuku badala ya mkopo kwa wachimbaji wadogo kutokana na wachimbaji wadogo kushindwa masharti ya mikopo na hivyo kushindwa kurejesha na badala yake sasa wanapewa ruzuku.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vipaumbele muhimu vinavyozingatiwa katika kutoa ruzuku hiyo ni pamoja na kumiliki leseni hai na halali ya shughuli za uchimbaji, kuwa na utambulisho wa kodi na mlipa kodi (TIN) na rekodi nzuri ya kulipa mrabaha na mapato mengine ya Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wakala wa Jiolojia Tanzania wataendelea kufanya utafiti wa maeneo yote nchini ili wachimbaji wadogo nao sasa waweze kunufaika na rasilimali hii ya Taifa.