Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 43 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 351 2017-06-07

Name

Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GIMBI D. MASABA aliuliza:-
Kampuni ya Group Sogesca Lanari Estero (GSLE) iliyokuwa inajenga barabara ya Nyanguge – Musoma kati ya mwaka 1979 – 1990 iliacha majengo katika Kijiji cha Yimtwila “A” ambapo Serikali kwa kushirikiana na wananchi wakaanzisha shule ya sekondari ya kutwa.
Je, ni kwa nini Serikali isitumie fursa ya uwepo wa majengo haya kupandisha hadhi shule hiyo kuwa ya kidato cha tano na sita kwa kuwa nyumba za walimu na mabweni yanaweza kupatikana?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Gimbi Dotto Masaba, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, majengo yaliyokuwa kambi ya Kampuni ya Group Sogesca Lanari Estero iliyokuwa inajenga barabara ya Nyanguge kwenda Musoma kati ya mwaka 1979 hadi 1990 kwa sasa yanatumika kwa ajili ya Shule ya Sekondari ya Sogesca ambayo ni ya kutwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kufanikisha uwepo wa shule ya kidato cha tano na sita Wilayani Busega, Serikali imeweka kipaumbele cha kuanzisha shule ya sekondari Mkula kuwa ya kidato cha tano na sita katika mwaka wa fedha 2016/2017. Tayari Serikali imepeleka shilingi milioni 259 kwa ajili ya ujenzi wa bweni la wanafunzi, vyumba vya madarasa vinne, matundu ya vyoo kumi na ukarabati wa maabara. Mpango wa Serikali ni kuhakikisha shule za sekondari za kidato cha tano na sita zinaanzishwa katika kila tarafa.