Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 06 2018-04-03

Name

Jaffar Sanya Jussa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Paje

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA (K.n.y. MHE. JAFFAR SANYA JUSSA) aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itavipatia Vituo vya Polisi vya Paje na Jambiani samani za ofisi pamoja na magari kwa ajili ya patrol?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jaffar Jussa, Mbunge wa Paje, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna uhaba wa magari pamoja na samani katika Vituo vya Polisi vya Paje na Jambiani, kama ilivyo kwenye maeneo mengine hapa nchini. Kwa sasa Vituo vya Polisi cha Paje na Jambiani vinapata huduma za doria kutoka kwa OCD wa Makunduchi, hali inayosababisha kuwa na changamoto katika utekelezaji wa majukumu ya kiusalama.
Mheshimiwa Naibu Spika, Jeshi la Polisi lipo katika mchakato wa kupokea magari mapya yaliyonunuliwa na Serikali ambayo yatagawawiwa kwa kuzingatia kiwango cha uhalifu, idadi ya watu na ukubwa wa eneo katika kamandi husika. Aidha, Jeshi la Polisi litaendelea kutumia bajeti inayotengwa kutimiza azma ya Serikali ya kuhakikisha kuwa linakuwa na vitendea kazi vya kutosha, ikiwa ni pamoja na magari na samani katika vituo vya Polisi kote nchini.