Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 70 2018-02-06

Name

Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELLE aliuliza:-
Ni Sera ya Taifa kuwa na Vituo vya Afya kwa kila Kata, na wananchi katika baadhi ya Kata wamejitahidi kujenga majengo kwa ajili ya vituo hadi kufikia usawa wa renta kwa nguvu zao:-
(a) Je, Serikali iko tayari kutoa fedha kwa ajili ya kukamilisha majengo ya vituo vya afya vya Ikobe, Ilolangulu, Kagera na Bukandwe?
(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza Watumishi wa Afya Wilayani Mbogwe?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Augustino Manyanda Maselle lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kutelekeza Sera ya Afya ya kuwa na kituo cha afya katika kila kata. Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe ina vituo viwili vya afya ambavyo ni Kituo cha Afya Iboya na Masumbwe, vituo vingine viwili vya Nhomolwa na Kagera viko katika hatua ya ukamilishaji wa ujenzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia uhisani wa Canada, Benki ya Dunia na Sweden imetoa kiasi cha shilingi milioni 800 kwa ajili ya kuboresha na kujenga miundombinu ya vituo vya afya vya Masumbwe na Iboya sawa na shilingi milioni 400 kwa kila kituo ili kuboresha huduma za mama na mtoto. Katika Mwaka wa Fedha 2017/2018, Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe imetenga kiasi cha shilingi milioni 35 kupitia ruzuku ya Maendeleo kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa majengo katika vituo vya afya Nhomolwa na Kagera pamoja na shilingi milioni 10 kwa ajili ya ukamilishaji wa jengo la wazazi katika zahanati ya Ilolangulu. Zahanati ya Bukandwe itatengewa fedha katika bajeti ya mwaka wa 2018/2019.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeajiri wataalam wa afya 2509 ambapo kati ya hao 16 walipangwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe na watumishi 13 wameripoti na kupangiwa vituo vya kazi. Serikali itaendelea kuajiri watumishi wa afya kadri wanavyohitimu na kupangwa moja kwa moja kwenye vituo.