Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 4 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 52 2018-02-02

Name

Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI aliuliza:-
Miongoni mwa Mahakama za Mwanzo ambazo Serikali iliahidi na kuamua kuzijenga ni pamoja na Mahakama ya Mwanzo Mkomazi. Je, ni lini Mahakama ya Mwanzo Mkomazi itajengwa?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niba ya Waziri wa Katibu na Sheria napenda kujibu swali la Mheshimiwa Stephen Hilary Ngonyani Mbunge wa Korogwe Vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mahakama ya Mwanzo ya Mkomazi ni moja ya Mahakama zilizo kwenye mpango wa ukarabati na ujenzi wa Mahakama za Mwanzo nchini. Hivyo, kwa mujibu wa mpango huo Mahakama ya Mwanzo Mkomazi imepangwa kujengwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020.