Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 51 2018-02-02

Name

Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA aliuliza:-
Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC) iliingia mkataba wa utafiti wa uchimbaji wa gesi na mafuta na Kampuni ya Mafuta ya Swala (SOGTP). Katika utekelezaji wa mpango huo wamegundua kuwepo kwa wingi mafuta ya petroli na gesi katika vijiji vya Kipenyo na Mtimbira Wilayani Malinyi katika Mkoa wa Morogoro.
(a) Je, ni lini uchimbaji wa visima na uvunaji wa mafuta utaanza rasmi katika maeneo hayo?
(b) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwatayarishia wananchi wa maeneo hayo ili kuondoa migogoro inayoweza kujitokeza baina yao na Serikali kama vile gesi ya Mtwara?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Hadji Hussein Mponda, Mbunge wa Malinyi, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, utafiti wa mafuta katika kitalu cha Kilosa – Kilombero unafanywa na Kampuni ya Swala Oil Gas Tanzania ulianza mwezi Februari, 2012. Utafiti huo ulianza baada ya kusainiwa kwa Mkataba wautafutaji kati ya Serikali kupitia TPDC na Swala mwezi Februari, 2012.
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo ambalo limeainishwa kwa ajili ya uchimbaji wa kisima hicho lipo katika Kijiji cha Ipera Asilia katika Hifadhi Tengefu ya Bonde la Kilombero.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kisima hicho kinatarajiwa kuanza kuchimbwa mwezi Septemba, 2018 kutegemea matokeo ya utafiti huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia TPDC imekuwa ikitoa elimu kwa wananchi wa maeneo kunakofanyika utafiti huo. Tarehe 06 hadi 17 Februari, 2017 TPDC kwa kushirikiana na Kampuni ya Swala ilitoa elimu ya masuala ya gesi na mafuta katika maeneo ya Halmashauri ya Mji huo ikiwa Mji Mkuu wa Mkoa wa Morogoro na Wilaya za Kilombero pamoja na Malinyi. Aidha, wananchi wa Kata ya Mtimbira, Njiwa pamoja na Kitete katika maeneo vijiji vya Mtimbira, Kipenyo, Ipera Asilia na Warama pia walipata elimu ya hifadhi ya mazingira pamoja na manufaa ya mradi huo.