Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 30 2018-02-01

Name

Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itapaleka madaktari na wauguzi katika Hospitali ya Wilaya ya Handeni hasa ikizingatiwa kuwa hali ya hospitali hiyo kwa sasa sio nzuri?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omari Abdallah Kigoda, Mbunge wa Handeni, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kupokea kibali cha ajira mwezi Julai, 2017 Serikali imepanga watumishi katika maeneo mbalimbali ili kupunguza tatizo la watumishi. Katika mgao huo Halmashauri ya Mji wa Handeni imepokea jumla ya watumishi 10 waliopangiwa vituo vya kazi Novemba, 2017. Watumishi waliopangiwa ni Daktari Daraja la II 1, Tabibu Wasaidizi wawili, Tabibu Meno mmoja, Wauguzi wawili, Afisa Muuguzi Msaidizi mmoja na Wateknolojia Wasaidizi Maabara wawili. Watumishi wote wamesharipoti na wanaendelea na kazi kama walivyopangiwa. Mgawanyo huu umefanyika ili kila eneo lipate wataalam.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na watumishi hao wapya, Halmashauri kwa kushirikiana na wadau wa afya inao watumishi 13 wanaofanya kazi kwa mikataba ya muda mfupi ambao wanafanya kazi katika Hospitali ya Wilaya Handeni. Aidha, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2018/2019 Halmashauri imeomba kibali cha kuajiri watumishi wa kada za afya 182 ili kukamilisha Ikama ya Idara ya Afya ya Halmashauri ya Mji Handeni. Serikali itaendelea kupanga watumishi kadri bajeti ya mishahara itakavyoruhusu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ambazo zimeathirika kwa kiwango kikubwa kinachoathiri utoaji wa huduma kwenye vituo vya kutolea huduma za afya kutokana na zoezi la uhakiki wa vyeti fake zinaelekezwa kuwasilisha maombi ya ajira mbadala moja kwa moja Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ili kuweza kutatua changamoto hiyo.