Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 27 2018-01-31

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:-
Jimbo la Same Mashariki lina Kata 14 lakini lina Kituo kimoja cha Polisi kilichopo Kata ya Maore na vituo vidogo vilivyopo Kata ya Ndungu na Kihurio; vituo vyote hivyo vipo katika tarafa moja yenye kata tano, kata nyingine tisa ambazo zipo katika tarafa mbili zilizoko mlimani na zipo mbali sana na vituo hivyo vya Polisi zinapata shida sana kutoa ripoti za uhalifu. Kwa kuwa wananchi wa tarafa hizo mbili za mlimani tayari wametenga maeneo ya kuweka vituo vya Polisi:-
(a) Je, Serikali ipo tayari kuanzisha Vituo vya Polisi katika Tarafa ya Mamba/Vunta na Tarafa ya Gonja?
(b) Kama Serikali ipo tayari kuanzisha Vituo hivyo vya Polisi, je, ni lini Polisi hao wataanza kazi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani, najibu swali la Mheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka, Mbunge wa Same Mashariki, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa kuwa na Vituo vya Polisi katika ngazi ya Kata na Tarafa nchi nzima, Mamba/Vunta na Gonja zikiwemo. Katika Tarafa ya Gonja kuna Kituo cha Polisi, Daraja B kinachotoa huduma za kipolisi katika eneo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Tarafa ya Mamba wananchi wamejitolea eneo hilo kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi ambapo kwa sasa majadiliano kati ya Jeshi la Polisi na wananchi kuhusu ujenzi wa Kituo cha Polisi, Daraja la B yanaendelea. Hata hivyo, kwa sasa Tarafa ya Mamba ina Kituo kidogo Daraja la C ambacho kinatoa huduma kwa wananchi katika Tarafa hiyo. Aidha, Jeshi la Polisi hufanya doria mara kwa mara katika maeneo hayo ya milimani ambayo hafikiwi kirahisi na vyombo vya usafiri kutokana na jiografia yake.