Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 2 Foreign Affairs and International Cooperation Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 26 2018-01-31

Name

Machano Othman Said

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. SAADA MKUYA SALUM (K.n.y MHE. MACHANO OTHMAN SAID) aliuliza:-
Kwa muda mrefu Tanzania imekuwa na uhusiano mzuri kiuchumi, kiafya na kisiasa na Jamhuriya Muungano wa Watu wa Cuba, lakini Tanzania haina Ubalozi katika nchi hiyo:-
(a) Je, ni lini Tanzania itafungua ubalozi wake nchini Cuba hasa ikizingatiwa kuwa Cuba tayari wana Ubalozi nchini muda mrefu?
(b) Je, Serikali inajua kwamba kutokana na Tanzania kutofunga Ubalozi nchini Cuba, imesababisha sanamu ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyeree kutowekwa katika uwanja wa Viongozi muhimu wa Afrika katika Jiji la Havana?

Name

Dr. Susan Alphonce Kolimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ruhusa yako na kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashaki, kabla ya kujibu swali la Mheshimiwa Machano Othman Said, Mbunge wa Baraza la Wawakilishi naomba kutoa maelezo mafupi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Tanzania na Cuba imekuwa na mahusiano mazuri ya Kidiplomasia, Kisiasa, Kiuchumi, Kielimu, Kiafya na Kiutamaduni kwa muda mrefu yalioanzishwa na waasisi wa Mataifa haya mawili, Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wa Tanzania na Hayati Fidel Alejandro Castro Ruz wa Cuba. Kwa ujumla mahusiano haya mazuri yamedumu kwa miaka mingi kutokana na kuwa na maslahi mapana na nchi yanayozingatia usawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maelezo haya mafupi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Machano Othman Said, Mbunge wa Baraza la Wawakilishi, lenye vipengele (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Tano kwa kutambua mahusiano mazuri na ya muda mrefu yaliyopo baina ya nchi hizi mbili ina mpango wa kufungua ubalozi katika Mji wa Havana Cuba. Hivi sasa taratibu za kufungua Balozi hizi zinaendelea, mara zitakapokuwa zimekamilika ubalozi huo utafunguliwa kama ulivyopangwa.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Cuba kwa kutambua na kuthamini mchango mkubwa uliotolewa na mashujaa katika vita vya ukombozi wa bara la Afrika iliamua kujenga mnara wa kumbukumbu kuenzi juhudi na harakati hizo pamoja uzalendo wa viongozi hao akiwemo Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.
Mheshimiwa Mwenyekiti, si kweli kwamba Tanzania kutokufungua Ubalozi nchini Cuba kumesababisha sanamu ya Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kutokuwekwa katika Uwanja wa Viongozi Muhimu Afrika katika Jiji la Havana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sanamu hiyo haikuwekwa katika uwanja huo kutokana na muonekano wake kutokuwa na uhalisia wa sura ya Hayati Baba wa Taifa, hivyo utengenezaji wake kuanza upya. Matengenezo ya sanamu hiyo yanaendelea na Serikali inafanya juhudi ili sanamu hiyo ikamilike na kuwekwa sehemu iliyopangwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kulithibitishia Bunge lako Tukufu kuwa mahusiano ya Tanzania na Cuba yataendelea kuwa mazuri katika nyanja mbalimbali hapa nchini kama vile diplomasia, afya, elimu, michezo, utalii na biashara.