Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 6 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 57 2016-04-27

Name

Joshua Samwel Nassari

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO (K.n.y. MHE. JOSHUA S. NASSARI) aliuliza:-
Shamba Na.112 (Ex-Arusha Coffee Estate) lililopo Nduruma Wilaya ya Meru lililokuwa likimilikiwa na Tanzania Flowers Ltd. lenye ukubwa wa ekari 721 lilishawahi kufutwa mwaka 2000 na hati ya utwaaji ardhi (Deed of Acquisition) ikasajiliwa 12/6/2001 na aliyekuwa Waziri wa Ardhi wa wakati huo, Mheshimiwa Gideon Cheyo lakini hadi leo wawekezaji hao bado wanazidi kuiuza ardhi hiyo ambayo ilifutwa kwa ajili ya kuwagawia wananchi wenye shida ya ardhi:-
Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya jambo hilo hasa ikizingatiwa kuwa Serikali ilishawahi kuwaambia wananchi wa maeneo hayo kuwa shamba hilo halimilikiwi na wawekezaji tena?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joshua Samwel Nassari, Mbunge wa Arumeru, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, shamba Na.112 lilikuwa na ukubwa wa ekari 721 na lilikuwa eneo la Nduruma, Wilaya ya Arumeru Mkoa wa Arusha. Tarehe 14/11/1990 shamba hili lilimilikishwa kwa Tanzania Flowers Ltd. ya Arusha na mnamo tarehe 8/8/1991 na tarehe 2/10/1991 kampuni hiyo ililigawa shamba hilo katika sehemu saba na kuwauzia watu sita tofauti baada ya kufuata taratibu zote za kisheria na sehemu moja yenye ekari 80 iliendelea kumilikiwa na Tanzania Flowers Ltd. Kampuni zilizouziwa zilipewa hati kutokana na hatimiliki mama yenye Na.7320 hili lilifanyika kwa kuzingatia kufungu cha Sheria Na. 83 na 88 cha Sheria ya Usajili wa Ardhi. Mgawanyo wa shamba hilo ulikuwa kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, tarehe 6/12/2011, Serikali iliamua kulitwaa eneo linalomilikiwa na Tanzania Flowers Limited lenye Hati Na. 7320 ambalo kwa wakati huo lilikuwa na ukubwa wa ekari 80. Utwaaji huu ulisajiliwa kwa Waraka Na.14316. Hivyo basi, ekari 80 zilitwaliwa kwa ajili ya matumizi ya wananchi, na ardhi hiyo ilisharudishwa kwa Halmashauri Halmashauri ya Arumeru ndiyo wanahusika katika ugawaji wa shamba hilo.