Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 18 2018-01-31

Name

Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. KASUKU S. BILAGO aliuliza:-
Walimu wa Elimu Maalum wanapohitimu kwenye Vyuo vya Patandi na SEKOMU hawapelekwi kwenye shule za vitengo vya elimu maalum:-
(a) Je, Serikali haioni kama inapoteza rasilimali fedha na watu kwa kutoa elimu isiyo na tija kwa Walimu hao?
(b) Je, ni lini Serikali itawapanga walimu wenye elimu maalum kwenye shule na vitengo vyenye mahitaji hayo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo alilosema Mheshimiwa Bilago halihusiani kabisa na swali lake. Hata hivyo, nataka kumwambia kwamba kukatika kwa mkanda si kuvuliwa kwa mkanda. Ahsante sana. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kasuku Samson Bilago, Mbunge wa Buyungu lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutoa mafunzo kwa Walimu ni miongoni mwa mikakati ya kuongeza tija ya kazi na ubora wa elimu inayotolewa, si kupoteza rasilimali fedha na rasilimaliwatu. Kwa muktadha huo, Chuo wa Walimu wa Elimu Maalum Patandi hudahili Walimu kutoka kazini ambao huhitimu kwa viwango vya astashahada na stashahada. Chuo Kikuu cha Elimu Maalum SEKOMU hudahili walimu kutoka kazini na pia Walimu wapya kwa kiwango cha shahada.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika vyuo vyote viwili, wahitimu waliodahiliwa kutoka kazini hurudi kwenye vituo vyao vya kazi wakisubiri uhamisho kwenda kwenye shule za vitengo vya elimu maalum; na wahitimu ambao hudahiliwa kabla ya ajira huajiriwa na Serikali na kupangiwa shule zenye vitengo vya elimu maalum na wengine huajiriwa na Sekta Binafsi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kati ya mwaka 2012 na 2015 Serikali iliajiri Walimu wapya 614 wa elimu maalum ambao walipangiwa kufundisha kwenye shule zenye vitengo vya elimu maalum. Hadi Desemba 2016 wapo Walimu 3,957 wa elimu maalum nchini sawa na asilimia 74.3 ya Walimu 5,324 wanaohitajika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuhakikisha Walimu wote wenye taaluma za elimu maalum wanatumika vizuri, nazielekeza Halmashauri zote ziwahamishie Walimu wa elimu maalum kwenye shule zenye vitengo vya elimu maalum ifikapo Desemba 31, 2018. (Makofi)