Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 96 2017-11-16

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. NAGU aliuliza:-
Mwaka 2014/2015 Serikali kupitia Agizo la Mheshimiwa Rais iliwataka wananchi kuchangia ujenzi wa maabara na wananchi waliitikia kwa kiasi kikubwa sana, hasa katika Wilaya ya Hanang:-
(a) Je, ni lini Serikali italeta vifaa vya maabara katika majengo hayo ya maabara yaliyokamilika katika Wilaya ya Hanang?
(b) Je, Serikali itasaidia vipi kukamilisha maabara ambazo kutokana na njaa wananchi hawakuweza kukamilisha ujenzi wake?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dokta Mary Michael Nagu, Mbunge wa Hanang, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Hanang ina jumla ya shule za sekondari 33 zenye mahitaji ya vyumba vya maabara 99 kwa ajili ya masomo ya sayansi. Ujenzi wa vyumba vya maabara katika shule 11 umekamilika kati ya 33 hizi zilizopo.
Mheshimiwa Spika, shule 10 zilizokamilisha ujenzi wa maabara kabla ya Januri 2017 zimepatiwa vifaa vya maabara. Shule moja haikupata vifaa vya maabara kwa kuwa, ilikamilisha ujenzi baada ya Januari 2017. Aidha, Serikali kupitia Mpango wa Elimu Msingi Bila Malipo inatoa fedha ambazo sehemu yake zinatakiwa kutumika kwa ajili ya kununua vifaa na kemikali za maabara. Katika kipindi cha kuanzia Disemba 2015 mpango ulipoanza kutekelezwa, Halmashauri ya Wilaya ya Hanang imepokea na kutumia Sh.253,913,281/= kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya maabara.
(b) Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2016/2017, zilitengwa shilingi milioni 70 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa maabara katika Shule za Sekondari za Hanang, ikiwepo Msqaroda, Bassodesh, Gidahababieg na Simbay. Vilevile katika Mwaka wa Fedha 2017/2018, zimetengwa jumla ya shilingi 233,564,900 kwa ajili ya kuendelea na ukamilishaji wa ujenzi wa maabara ambazo hazijakamilika. Kati ya fedha hizo, shilingi milioni 80 zinatokana na makusanyo ya ndani ya halmashauri na shilingi 153,564,900 ni ruzuku kutoka Serikali Kuu kwa maana ya CDG.