Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 3 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 36 2017-11-09

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Primary Question

MHE. DOTO M. BITEKO aliuliza:-
Askari wa Wilaya ya Bukombe wanazo changamoto nyingi zikiwemo ukosefu wa nyumba za askari.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia nyumba askari hao katika Wilaya ya Bukombe?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu Sali la Mheshimiwa Doto Mashaka Biteko, Mbunge wa Bukombe kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli Jeshi la Polisi lina changamoto mbalimbali ikiwemo uchache wa nyumba za kuishi askari. Wilaya ya Bukombe ambayo ina jumla ya maafisa wakaguzi na askari 122 ni miongoni mwa Wilaya zenye changamoto za uhaba wa nyumba za kuishi askari.
Mheshimiwa Spika, Serikali ina mpango wa kujenga nyumba za kuishi askari katika mikao ya wialaya kwa awamu. Katika Wilaya ya Bukombe, Jeshi la Polisi lipo kwenye mazungumzo na Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe ili kupatiwa eneo kwa ajili ya kujenga nyumba za kuishi askari. Baada ya kupatiwa eneo hilo Serikali itajenga nyumba hizo kwa fedha za bajeti kwa kadri fedha zitakavyopatikana kwa jinsi ilivyotengwa pamoja na kushirikiana na wadau wengine wa maendeleo.