Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 1 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 14 2017-11-07

Name

Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. IGNAS A. MALOCHA aliuliza:-
Katika bajeti ya 2016/2017 Serikali ilipanga kujenga baadhi ya Mahakama za Wilaya na za Mwanzo katika maeneo mbalimbali nchini.
(a) Je, ni hatua ipi imefikiwa katika ujenzi wa Mahakama hizo?
(b) Kwa kuwa Mahakama ya Mwanzo Mtowisa katika Wilaya ya Sumbawanga Vijijini ni miongoni mwa Mahakama iliyopangiwa bajeti ya ujenzi kutokana na uchakavu mkubwa na hatarishi kwa wananchi, je, ni lini ujenzi utaanza?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU - KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA) alijiibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ignas Aloyce Malocha, Mbunge wa Kwela, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli Mahakama imepanga kujenga na kukarabati majengo yake katika maeneo mbalimbali nchini. Mahakama imejiwekea mpango wa kujenga na kukarabati majengo hayo kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Utekelezaji wa mpango huu unaendelea.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2017/2018 Mahakama imepanga kujenga Mahakama Kuu Kigoma na Mara na kufanya ukarabati mkubwa wa jengo la Mahakama Kuu Sumbawanga. Aidha, kwa upande wa Mahakama za Hakimu Mkazi, kipaumbele kimetolewa katika Mikoa ya Simiyu, Njombe, Katavi, Manyara, Lindi na Geita.
Mheshimiwa Spika, vilevile Serikali imepanga kujenga Mahakama za Wilaya na za Mwanzo katika maeneo mbalimbali nchini. Mahakama ya Mwanzo Mtowisa ni moja ya maeneo yaliyopangwa kujengwa na ujenzi utaanza mara moja baada ya upatikanaji wa fedha za maendeleo.
Mheshimiwa Spika, katika mpango wa Mahakama wa kujenga majengo kwenye Mikoa mbalimbali, kikwazo kimekuwa ni upatikanaji wa viwanja pamoja na hati miliki za viwanja.